Psalms 11

Kumtumaini Bwana

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi)


1 aKwa Bwana ninakimbilia,
unawezaje basi kuniambia:
“Ruka kama ndege kwenye mlima wako.

2 bHebu tazama, waovu wanapinda pinde zao,
huweka mishale kwenye uzi wake,
wakiwa gizani ili kuwapiga
wale wanyofu wa moyo.

3 cWakati misingi imeharibiwa,
mwenye haki anaweza kufanya nini?”


4 d Bwana yuko ndani ya Hekalu lake takatifu;
Bwana yuko kwenye kiti chake cha enzi mbinguni.
Huwaangalia wana wa watu,
macho yake yanawajaribu.

5 e Bwana huwajaribu wenye haki,
lakini waovu na wanaopenda jeuri,
nafsi yake huwachukia.

6 fAtawanyeshea waovu makaa ya moto mkali
na kiberiti kinachowaka,
upepo wenye joto kali ndio fungu lao.


7 gKwa kuwa Bwana ni mwenye haki,
yeye hupenda haki.
Wanyofu watauona uso wake.
Copyright information for SwhKC